Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan - Lipi Lenye Faida Zaidi; Kulingania Katika Da'awah Au Kutafuta Elimu Kwanza?

Lipi Lenye Faida Zaidi; Kulingania Katika Da'awah Au Kutafuta Elimu Kwanza?

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

  
SWALI:

Ni jambo lipi katika haya mawili ni bora? Kutafuta elimu au kulingania watu kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Kwa sababu nilisikia baadhi ya makundi yakisema: "Da'wah kwa ajili ya Allaah ni yenye faida kubwa kulikoni kutafuta elimu."


JIBU:

Kutafuta elimu ni jambo la mwanzo kabisa, kwa sababu haiwezekani mtu kuweza kuwalingania watu katika Dini ya Allaah mpaka awe na elimu; ama akiwa hana elimu basi hawezi kuwalingania watu katika Dini ya Allaah, na ikiwa atafanya (Da'wah) basi atakayokosea yatakuwa makubwa zaidi kuliko atakayopatia. Kwa hiyo, ni sharti kwa Mlinganiaji kuwa na elimu kabla ya kuanza kulingania watu; haya ni kutokana na kauli Yake Allaah:

قُلْ هَـٰذِهِ سَبِيلِي أَدْعُو إِلَى اللَّـهِ ۚ عَلَىٰ بَصِيرَةٍ أَنَا وَمَنِ اتَّبَعَنِي ۖ وَ سُبْحَانَ اللَّـهِ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُشْرِكِينَ
Sema: “Hii ndio njia yangu nalingania kwa Allaah, juu ya baswiyrah (nuru ya elimu, ujuzi, umaizi) mimi na anayenifuata. Na Subhaana-Allaah (Utakasifu ni wa Allaah), nami si miongoni mwa washirikina.” [Yuwsuf: 108]

Hata hivyo; kwa mambo ya wazi (yanayojulikana na kila mmoja) Inawezekana kwa mtu wa kawaida kulingania katika mambo hayo; kama kuamrisha Swalaah na kukataza kuipuuza (Swalaah), kuamrisha Swalaah ya Jamaa’ah (kwa wanaume), kuamrisha watoto kuswali; mambo haya yanafahamika kwa (wote); mtu wa kawaida na mtafutaji elimu.

Hata hivyo; mambo ambayo yanahitaji ufahamu na ujuzi kuhusu Halaal na Haraam na mambo ya Shirk na Tawhiyd, hayo basi lazima kutafutwe elimu katika hayo. Kwa ujumla, wote wanaosema ya kuwa; Kufanya Da'wah ni jambo lenye kunufaisha kulikoni kusoma, hao ni Jamaa’at At-Tabliygh na hao ni katika kundi potofu la uzushi la Kisufi.


[Al-Ijaabat Al-Faaswilat 'Alaa Ash-Shubuhaat Al-Haaswilah, uk. 20

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MTAMBUE JINI MAHABA NA TIBA YAKE

ASALAMU ALAYKUM M aisha ya mwanadamu yamezungukwa na misukos uko na mitihani mbalimbali ambayo wakati mwingine humfanya ajione tofauti na kujiona mwenye kukosa thamani ya maisha, miongoni mwa matatizo ambayo huyapata wengi katika ulimwengu tulionao ni tatizo la jini mahaba nalo huwa pa watu weng i fadhaiko na kukosa amani na raha ya maisha  JINI MAHABA NI NINI? J ini mahaba ni jini {pepo,shetani} yeyote alie muingia mwanaadamu kwa lengo la kufanya nae uchafu wa zinaa. VIPI ANAWEZA KUMUINGIA MTU?     J ini mahaba hu waingia watu kwa sababu nyingi m iongoni mwazo ni kulala bila ya nguo au nguo nye pesi sana bila ya kusoma dua hasa nyakati za jo to 2.wakati wa kufanya tendo la ndoa na wanandoa kusahau kusoma dua wakati wa tendo{na hapa ndipo huwaingia watu zaidi} 3.kujitazama ktk kioo kwa muda mrefu bila ya kusoma dua na hasa kwa wanaopenda kujitazama waki wa uchi 4.kuogelea ukiwa uchi katika vyanzo vya maji bila ya dua {hii hupelekea kuingiwa hasa ...

TIBA YA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

ASALAMU ALAYKUM     katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya jiji la dar na ulimwengu kwa ujumla imekuwa ni jambo la kawaida kuona mara kwa mara uuzwaji wa zinazoitwa dawa za kuongeza nguvu za kiume            jambo ambaloz amani halikuwepo kwani watu waliweza kuwa na nguvu za kutosha kulimudu tendo la ndoa bila kuhitajia dawa yoyote ile leo imekuwa kama desturi kama hujui dawa ya nguvu za kiume wewe hutakuwa mganga na hutapata mtu wa kumtibu kwani ni zaidi ya asilimia 60% ya wtakao hitaji tiba watahitaji dawa ya nguvu za kiume jambo lililonipelekea kuandika makala hii ambayo nataraji itakuwa na manufaa kwa wengi  NGUVU ZA KIUME Ni hali ya mtu kuweza kumudu tendo la ndoa na kiasili hakuna ugonjwa wa nguvu za kiume bali kuna upungufu wa nguvu za kiume NINI CHANZO CHA TATIZO HILI kuna sababu nyingi znazopelekea upungufu wa nguvu za kiume miongoni mwazo ni; kuugua kwa mu...

FAIDA ZA KITUNGUU SWAUM

KITUNGUU THAUM (Swaumu/Saumu): Moja ya mmea ambao umependelewa sana na Mungu kwakuwa na viinilishe vingi na mhimu sana kwa afya ya binadamu ni kitunguu swaumu. Kitunguu swaumu ni dawa karibu kwa kila ugonjwa. Kitunguu swaumu ni jamii ya vitunguu ambayo kwa kitaalamu huitwa Allium sativum . Jamii hii ilianza kutumika katika mabara mbalimbali duniani hususani Asia, Afrika na Ulaya takribani miaka 6000 iliyopita. Matumizi makuu nyakati hizo yakiwa viungo katika mboga na tiba. Kitunguu swaumu kimetajwa kwenye vitabu mbalimbali vya dini vikielezea faida zake katika kutibu maradhi mbalimbali yasababishwayo na bakteria, matatizo katika mapafu, matatizo katika mfumo wa umen’genyaji chakula, na matatizo ya kuishiwa nguvu. Historia inaonyesha kuwa, vitunguu swaumu vilianza kutumika nchini China mwaka 510 kabla ya Kristo na pia vilitumiwa na wanajeshi wa Ugiriki na Warumi. Aidha wasafiri wa vyombo vya baharini na vijijini pamoja na wakulima barani Afrika walivitumia sana. Kuna baadhi ya ...